Surah Al-'adiyat (Those That Run)

Listen

Swahili

Surah Al-'adiyat (Those That Run) - Aya count 11

وَٱلۡعَـٰدِیَـٰتِ ضَبۡحࣰا ﴿١﴾

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,

Ninaapa kwa farasi wa Jihadi wendao mbio, na huku pumzi zao zinasikilizana kwa sauti inayo itwa "Dh'abh'an".


Arabic explanations of the Qur’an:

فَٱلۡمُورِیَـٰتِ قَدۡحࣰا ﴿٢﴾

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,

Na kwa farasi hao ambao hutoa cheche za moto zinapo gonga kwato zao kwenye ardhi wanapo kwenda.


Arabic explanations of the Qur’an:

فَٱلۡمُغِیرَ ٰ⁠تِ صُبۡحࣰا ﴿٣﴾

Wakishambulia wakati wa asubuhi,

Na kwa farasi hao wanao washambulia maadui asubuhi kabla jua halijachomoza;


Arabic explanations of the Qur’an:

فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعࣰا ﴿٤﴾

Huku wakitimua vumbi,

Wakatimua mavumbia mengi, farasi hao, kati ya makundi ya maadui!


Arabic explanations of the Qur’an:

فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا ﴿٥﴾

Na wakijitoma kati ya kundi,

Ikawa vumbi limewagubika maadui hata wakaingiwa kiwewe na kufazaika.


Arabic explanations of the Qur’an:

إِنَّ ٱلۡإِنسَـٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودࣱ ﴿٦﴾

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!

Hakika mwanaadamu ni mwingi wa kuzikufuru neema za Mola wake Mlezi ambazo hazikadiriki.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَ ٰ⁠لِكَ لَشَهِیدࣱ ﴿٧﴾

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka atakuwa mwingi wa kuja jishuhudia huko Akhera kwa kuungama madhambi yake.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَیۡرِ لَشَدِیدٌ ﴿٨﴾

Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!

Na hakika yeye kwa uchoyo na kuyapenda mali alio nayo, ni bakhili, hatoi kama inavyo mwajibikia katika mali yake.


Arabic explanations of the Qur’an:

۞ أَفَلَا یَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِی ٱلۡقُبُورِ ﴿٩﴾

Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?

Kwani hajui mwisho wa hali yake, hata hajui wakitolewa maiti waliomo makaburini,


Arabic explanations of the Qur’an:

وَحُصِّلَ مَا فِی ٱلصُّدُورِ ﴿١٠﴾

Na yakakusanywa yaliomo vifuani?

Na vikakusanywa viliomo vifuani navyo vimekwisha sajiliwa katika madaftari yao, yakiwa mema au mabaya waliyo yatenda?


Arabic explanations of the Qur’an:

إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ یَوۡمَىِٕذࣲ لَّخَبِیرُۢ ﴿١١﴾

Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!

Kwamba hakika Mlezi wao na Muumba wao bila ya shaka anajua vyema vitendo vyao na malipo yao Siku ya Kufufuliwa na Kulipwa.


Arabic explanations of the Qur’an: