Surah Al-Qari'ah (The Striking Hour)

Listen

Swahili

Surah Al-Qari'ah (The Striking Hour) - Aya count 11

ٱلۡقَارِعَةُ ﴿١﴾

Inayo gonga!

AL-QAARIA'H, Inayo gonga, ni Kiyama, ambacho kinaanza kwa mpulizo wa mwanzo wa barugumu, na kinaishia itapo katwa hukumu baina ya watu.


Arabic explanations of the Qur’an:

مَا ٱلۡقَارِعَةُ ﴿٢﴾

Nini Inayo gonga?

Kitu gani kilicho cha ajabu zaidi katika ukuu wake, na khatari zake na kitisho chake!


Arabic explanations of the Qur’an:

وَمَاۤ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ ﴿٣﴾

Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?

Na kitu gani kitacho kujuulisha hali ya AL-QAARIA'H katika kitisho chake juu ya nafsi za watu?


Arabic explanations of the Qur’an:

یَوۡمَ یَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ ﴿٤﴾

Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;

Siku hiyo watu watakuwa kama vipepeo kwa wingi na kuhangaika kulia na kushoto, madhaifu na wanyonge!


Arabic explanations of the Qur’an:

وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ ﴿٥﴾

Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!

Na milima itakuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na kuchambuliwa kwa kutapanyika vipande mbali mbali na kupeperuka katika anga huku na huku.


Arabic explanations of the Qur’an:

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَ ٰ⁠زِینُهُۥ ﴿٦﴾

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,

Ama yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, mema yake yakapindukia kuliko maovu yake,


Arabic explanations of the Qur’an:

فَهُوَ فِی عِیشَةࣲ رَّاضِیَةࣲ ﴿٧﴾

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.

Basi huyo atakuwa na maisha yatayo mridhisha mwenyewe, na nafsi yake itue.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَ ٰ⁠زِینُهُۥ ﴿٨﴾

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,

Na ama ambaye mizani yake itakuwa nyepesi, na maovu yake yakazidi kuliko mema yake,


Arabic explanations of the Qur’an:

فَأُمُّهُۥ هَاوِیَةࣱ ﴿٩﴾

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!

Basi makaazi yake yatakuwa Jahannamu.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَمَاۤ أَدۡرَىٰكَ مَا هِیَهۡ ﴿١٠﴾

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?

Na nini cha kukujuulisha ni nini Hawiya?


Arabic explanations of the Qur’an:

نَارٌ حَامِیَةُۢ ﴿١١﴾

Ni Moto mkali!

Moto ulio mkali, hapana moto unao fikilia ukali wake, hata ukichochewa vipi na kutiwa kuni gani!


Arabic explanations of the Qur’an: