Surah Al-Humazah (The Slanderer)

Listen

Swahili

Surah Al-Humazah (The Slanderer) - Aya count 9

وَیۡلࣱ لِّكُلِّ هُمَزَةࣲ لُّمَزَةٍ ﴿١﴾

Ole wake kila safihi, msengenyaji!

Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.


Arabic explanations of the Qur’an:

ٱلَّذِی جَمَعَ مَالࣰا وَعَدَّدَهُۥ ﴿٢﴾

Aliye kusanya mali na kuyahisabu.

Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.


Arabic explanations of the Qur’an:

یَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥۤ أَخۡلَدَهُۥ ﴿٣﴾

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!

Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?


Arabic explanations of the Qur’an:

كَلَّاۖ لَیُنۢبَذَنَّ فِی ٱلۡحُطَمَةِ ﴿٤﴾

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.

Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!


Arabic explanations of the Qur’an:

وَمَاۤ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ ﴿٥﴾

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?

Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?


Arabic explanations of the Qur’an:

نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ ﴿٦﴾

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!


Arabic explanations of the Qur’an:

ٱلَّتِی تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ ﴿٧﴾

Ambao unapanda nyoyoni.

Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.


Arabic explanations of the Qur’an:

إِنَّهَا عَلَیۡهِم مُّؤۡصَدَةࣱ ﴿٨﴾

Hakika huo utafungiwa nao

Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani


Arabic explanations of the Qur’an:

فِی عَمَدࣲ مُّمَدَّدَةِۭ ﴿٩﴾

Kwenye nguzo zilio nyooshwa.

Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.


Arabic explanations of the Qur’an: