Surah Al-Fil (The Elephant)

Listen

Swahili

Surah Al-Fil (The Elephant) - Aya count 5

أَلَمۡ تَرَ كَیۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَـٰبِ ٱلۡفِیلِ ﴿١﴾

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?

Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.


Arabic explanations of the Qur’an:

أَلَمۡ یَجۡعَلۡ كَیۡدَهُمۡ فِی تَضۡلِیلࣲ ﴿٢﴾

Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?

Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَأَرۡسَلَ عَلَیۡهِمۡ طَیۡرًا أَبَابِیلَ ﴿٣﴾

Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,

Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.


Arabic explanations of the Qur’an:

تَرۡمِیهِم بِحِجَارَةࣲ مِّن سِجِّیلࣲ ﴿٤﴾

Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,

Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.


Arabic explanations of the Qur’an:

فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفࣲ مَّأۡكُولِۭ ﴿٥﴾

Akawafanya kama majani yaliyo liwa!

Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.


Arabic explanations of the Qur’an: