Surah Al-Ma'un (Small Kindnesses)

Listen

Swahili

Surah Al-Ma'un (Small Kindnesses) - Aya count 7

أَرَءَیۡتَ ٱلَّذِی یُكَذِّبُ بِٱلدِّینِ ﴿١﴾

Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?

Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?


Arabic explanations of the Qur’an:

فَذَ ٰ⁠لِكَ ٱلَّذِی یَدُعُّ ٱلۡیَتِیمَ ﴿٢﴾

Huyo ndiye anaye msukuma yatima,

Ukitaka kumjua basi ni huyo ambaye anaye msukuma yatima kwa nguvu, na anamtumilia mabavu, na anamdhulumu,


Arabic explanations of the Qur’an:

وَلَا یَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِینِ ﴿٣﴾

Wala hahimizi kumlisha masikini.

Na wala hahimizi kulishwa masikini.


Arabic explanations of the Qur’an:

فَوَیۡلࣱ لِّلۡمُصَلِّینَ ﴿٤﴾

Basi, ole wao wanao swali,

Maangamio yatawashukia wanao sali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.


Arabic explanations of the Qur’an:

ٱلَّذِینَ هُمۡ عَن صَلَاتِهِمۡ سَاهُونَ ﴿٥﴾

Ambao wanapuuza Sala zao;

Maangamio yatawashukia wanao swali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.


Arabic explanations of the Qur’an:

ٱلَّذِینَ هُمۡ یُرَاۤءُونَ ﴿٦﴾

Ambao wanajionyesha,

Ambao huonyesha kwa watu vitendo vyao, ili wapate cheo katika nyoyo za hao watu, na wasifiwe.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَیَمۡنَعُونَ ٱلۡمَاعُونَ ﴿٧﴾

Nao huku wanazuia msaada.

Na huku wanazuia hisani zao na msaada wao kwa watu


Arabic explanations of the Qur’an: