Surah Al-Masad (The Palm Fibre)

Listen

Swahili

Surah Al-Masad (The Palm Fibre) - Aya count 5

تَبَّتۡ یَدَاۤ أَبِی لَهَبࣲ وَتَبَّ ﴿١﴾

Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.

Imeteketea mikono ya Abu Lahab iliyo kuwa ikiwaudhi Waislamu, na yeye mwenyewe amehiliki pia.


Arabic explanations of the Qur’an:

مَاۤ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ ﴿٢﴾

Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.

Hayatolindwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu mali yake aliyo kuwa nayo, wala cheo chake alicho kichuma.


Arabic explanations of the Qur’an:

سَیَصۡلَىٰ نَارࣰا ذَاتَ لَهَبࣲ ﴿٣﴾

Atauingia Moto wenye mwako.

Ataingia katika Moto unao waka, aungue.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ ﴿٤﴾

Na mkewe, mchukuzi wa kuni,

Na ataingia pia kwenye Moto mkewe huyo aliye kuwa akibeba masengenyo baina ya watu, kama alivyo ingia yeye (mumewe).


Arabic explanations of the Qur’an:

فِی جِیدِهَا حَبۡلࣱ مِّن مَّسَدِۭ ﴿٥﴾

Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.

Juu ya shingo yake itakuwa kamba ya mtende ya kumtesa.


Arabic explanations of the Qur’an: