Surah Al-Falaq (The Daybreak)

Listen

Swahili

Surah Al-Falaq (The Daybreak) - Aya count 5

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ ﴿١﴾

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,

Sema najikinga na Mola Mlezi wa asubuhi inapo pambazuka kutokana na usiku.


Arabic explanations of the Qur’an:

مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ﴿٢﴾

Na shari ya alivyo viumba,

Na shari ya kila chenye shari katika viumbe, ambavyo hapana wa kuzuia shari yao ila Mwenye kumiliki amri yao.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ ﴿٣﴾

Na shari ya giza la usiku liingiapo,

Na shari ya usiku unapo kuwa totoro.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَـٰتِ فِی ٱلۡعُقَدِ ﴿٤﴾

Na shari ya wanao pulizia mafundoni,

Na shari ya anaye pita baina ya watu kwa sababu ya kuwafisidi.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ ﴿٥﴾

Na shari ya hasidi anapo husudu.

Na shari ya hasidi anaye tamani iondoke neema kwa wengine.


Arabic explanations of the Qur’an: