Surah An-Nas (Mankind)

Listen

Swahili

Surah An-Nas (Mankind) - Aya count 6

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ ﴿١﴾

Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu,

Sema: Najikinga na Mola Mlezi wa wanaadamu, Mwenye kuendesha mambo yao.


Arabic explanations of the Qur’an:

مَلِكِ ٱلنَّاسِ ﴿٢﴾

Mfalme wa wanaadamu,

Mfalme wa wanaadamu, kwa ufalme ulio timia, kuwamiliki wote wafalme wao na maraia.


Arabic explanations of the Qur’an:

إِلَـٰهِ ٱلنَّاسِ ﴿٣﴾

Mungu wa wanaadamu,

Mungu wa wanaadamu, Mwenye uweza kwa kuwasarifu kwa ukamilifu atakavyo.


Arabic explanations of the Qur’an:

مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ ﴿٤﴾

Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,

Na shari ya mwenye kutia wasiwasi watu, ambaye hurudi nyuma ukiomba msaada kwa Mwenyezi Mungu dhidi yake.


Arabic explanations of the Qur’an:

ٱلَّذِی یُوَسۡوِسُ فِی صُدُورِ ٱلنَّاسِ ﴿٥﴾

Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,

Ambaye hutia kwa kificho katika vifua vya watu ya kuwaachisha wasende kwenye njia ya uwongofu.


Arabic explanations of the Qur’an:

مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ ﴿٦﴾

Kutokana na majini na wanaadamu.

Kutokana na majini na wanaadamu.


Arabic explanations of the Qur’an: