Surah Ad-Dhuha (The Forenoon)

Listen

Swahili

Surah Ad-Dhuha (The Forenoon) - Aya count 11

وَٱلضُّحَىٰ ﴿١﴾

Naapa kwa mchana!

Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!


Arabic explanations of the Qur’an:

وَٱلَّیۡلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

Na kwa usiku unapo tanda!

Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!


Arabic explanations of the Qur’an:

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَلَلۡـَٔاخِرَةُ خَیۡرࣱ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ ﴿٤﴾

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَلَسَوۡفَ یُعۡطِیكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰۤ ﴿٥﴾

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.


Arabic explanations of the Qur’an:

أَلَمۡ یَجِدۡكَ یَتِیمࣰا فَـَٔاوَىٰ ﴿٦﴾

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?


Arabic explanations of the Qur’an:

وَوَجَدَكَ ضَاۤلࣰّا فَهَدَىٰ ﴿٧﴾

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?


Arabic explanations of the Qur’an:

وَوَجَدَكَ عَاۤىِٕلࣰا فَأَغۡنَىٰ ﴿٨﴾

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?


Arabic explanations of the Qur’an:

فَأَمَّا ٱلۡیَتِیمَ فَلَا تَقۡهَرۡ ﴿٩﴾

Basi yatima usimwonee!

Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,


Arabic explanations of the Qur’an:

وَأَمَّا ٱلسَّاۤىِٕلَ فَلَا تَنۡهَرۡ ﴿١٠﴾

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,


Arabic explanations of the Qur’an:

وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ ﴿١١﴾

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.

Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.


Arabic explanations of the Qur’an: