Surah As-Sharh (The Opening Forth)

Listen

Swahili

Surah As-Sharh (The Opening Forth) - Aya count 8

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ ﴿١﴾

Hatukukunjulia kifua chako?

Hakika tumekukunjulia kifua chako kwa kuwa tulitia ndani yake Uwongofu na Imani.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ ﴿٢﴾

Na tukakuondolea mzigo wako!

Na tumekupunguzia mizigo iliyo kuwa mizito juu ya mgongo wako, kwa kukuunga mkono na kukusahilishia mambo yako,


Arabic explanations of the Qur’an:

ٱلَّذِیۤ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ ﴿٣﴾

Ulio vunja mgongo wako?

Ambayo yalikuwa ni mazito juu ya mgongo wako.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ ﴿٤﴾

Na tukakunyanyulia utajo wako?

Na tumelitukuza jina lako, tukalifanya linatajwa na ulimi wa kila Muumini pamoja na jina letu.


Arabic explanations of the Qur’an:

فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ یُسۡرًا ﴿٥﴾

Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi!

Hizo ni baadhi ya neema zetu juu yako. Basi kuwa na yakini na uweza wa Mwenyezi Mtukufu, kwani pamoja na uzito upo wepesi mwingi unao kuja nao.


Arabic explanations of the Qur’an:

إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ یُسۡرࣰا ﴿٦﴾

Hakika pamoja na uzito upo wepesi.

Hakika pamoja na uzito (wakati huo huo ijapo kuwa wewe hujui), upo wepesi mwingi vile vile.


Arabic explanations of the Qur’an:

فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ ﴿٧﴾

Na ukipata faragha, fanya juhudi.

Basi ukipata nafasi katika kazi ya kuwalingania watu, na mambo yaliyo khusiana na Jihadi, endelea na jitihada ya ibada na jishughulishe nafsi yako katika hayo.


Arabic explanations of the Qur’an:

وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب ﴿٨﴾

Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.

Kwa Mola wako Mlezi tu ndio uelekee kwa kumwomba na kumhitajia.


Arabic explanations of the Qur’an: